MASHABIKI NA WAPENZI WA KLABU YA SOKA YA JAMUHURI YENYE MASKANI YAKE MITAA YA CHASASA WETE PEMBA WAMESIFU USAJILI ULIOFANYWA NA UONGOZI WA KLABU ##

Mashabiki na wapenzi wa klabu ya soka ya Jamuhuri yenye maskani yake mitaa ya Chasasa Wete  Pemba wamesifu usajili uliofanywa na Uongozi wa klabu hiyo lakini wakasema bado tatizo linaloikabili klabu hiyo kongwe ni benchi la ufundi .

Wakizungumza  na mwandishi wa habari kwenye mazoezi ya klabu hiyo yanayoendelea katika  uwanja wa Utaani mashabiki hao wamesema kuwa usajili uliofanywa ni mzuri na unawapa matumaini ya klabu yao kurejea ligi kuu ya Zanzibar kwa msimu ujao .

Wameutaka Uongozi wa klabu kuhakikisha kwamba wanatafuta kocha mwenye uwezo na ambaye mbinu atakazowapa zitakuwa ni chachu ya ushindi wa klabu kwenye michuano ya Ligi daraja la kwanza Taifa Pemba baada ya kushuka daraja msimu uliopita .

“Usajili ni mzuri na wachezaji wote wanaonyesha kiwango lakini bado tatizo ni kocha mwenye uwezo na sifa za kufundisha timu , ni vyema uongozi ukatafuta kocha ambaye atakuwa ni chachu ya ushindi wa klabu yetu ”alieleza shabiki aliyejitambulisha kwa jina la Khamis .

Hata hivyo nahodha wa timu hiyo Mfaume Shaban ameutetea uongozi wa klabu na kusema kuwa kocha aliyepo anatosha na kuongeza kwamba wachezaji wenyewe wanatakiwa kujituma na kujitoa kwa ajili ya timu yao wawapo uwanjani .

“Hata kama atakuja kocha Ulaya  lakini wachezaji kama hawatakuwa na moyo wa kujituma basi mafanikio yatakuwa mbali cha msingi ni wachezaji kutambua wajibu na dhamana waliyonayo kwa klabu na mashabiki wao ”alisisitiza Mfaume .

Mafaume amewataka mashibi na wapenzi wa klabu hiyo kumwamini kocha aliyepo kwani anauwezo wa kuirejesha timu ligi Kuu ya Zanzibar msimu ujao na kuwaomba wachezaji  na mashabiki kuwa kitu kimoja ikiwa ni pamoja na kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu unapokuwa uwanjani .

Kwa upande wake Meneja wa Klabu hiyo Mohammed Abdalla Elisha amesema kuwa kwa kipindi hichi timu itaendelea kuwa chini ya kocha Hamad Mzee akisaidiwa na Ameir Chuwan na Juma Chande huki Ayoub Khamis Gopi akiwa ni kocha wa makipa .

Timu ya Soka ya Jamuhuri inatarajia kushuka kwenye  kiwanja cha Polisi Finya kucheza na timu ya Algezeera katika michuano ya ligi daraja la kwanza Taifa Pemba ikiwa imepangwa kundi moja na klabu ya Chipukizi FC  .
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment