Marehemu Almasi
Abdallah Shija alifariki akiwa anauguzwa
Tanga siku ya jumatatu tarehe 8 mwezi wa
8 2016 akiwa na umri wa miaka 32 na
amezikwa leo katika makaburi ya pangani kibaha maili moja.
Aidha kwa
mujibu wa taarifa kutoka kwa wanafamilia marehemu alifariki kutokana na
kupungukiwa damu tatizo ambalo limemchukua muda mrefu takribani miaka miwili hali
iliyompelekea kutoweza kufanya kazi akiwa ni mtu wa kukaa ndani na kuhitaji
uangalizi wa karibu.
Katika hatua
za mwisho marehemu alishindwa hata kunyanyuka mwenyewe kutokana na kukosa nguvu na eneo la chini kuanzia kwenye
kiuno kushindwa kufanya kazi .
Enzi za uhai
wake marehemu alikuwa ni moja kati ya watangazaji wa Mwambao fm Tanga 106.1 Tanzania.
“Trustedmishen blog”
kupitia kwa CEO N.E.C.H.I Inapenda kutoa pole kwa ndugu na jamaa wote wa
karibu walioguswa kwa namna moja au nyingine na msiba wa ndugu yetu Almasi
Abdallah Shija .
|
Marehemu
Almasi Abdallah Shija enzi za uhai wake |
|
Kushoto Almasi Abdallah Shija enzi za uhai wake akiwa na mfanyakazi mwenzie Jonas Msangi |
|
Marehemu wa kwanza kulia |
|
Moja kati ya vijana waliofundishwa kwa vitendo na marehemu katika tasnia ya uandishi wa habari Prisillah kushoto ,almasi kulia. |
“MUNGU AMPUMZISHE KWA AMANI,
TULIMPENDA ILA YEYE KAMPENDA ZAIDI”
‘Inna
lillahi wa inna ilaihi raji'un’
Mbaraka shijah mdogo wake marehemu
Yasini Shahibu Ali (K WA BONGE Tanzanian
artist ) Mjomba wake Marehemu
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
HAKIKA NI MAJONZI, ILA MAPENZI YA MUNGU NAYATIMIZWE, NA HAKI YAKE ITATENDEKA DAIMA
ReplyDelete