Huenda rapper AKA wa Afrika Kusini akapata shavu kwenye tamthilia ya Empire msimu ujao.
Waigizaji wa show hiyo iliyotokea kupendwa duniani, Taraji P Henson
(Cookie) na Terrance Howard (Lucious Lyon) wapo Afrika Kusini katika
ziara maalum iliyoandaliwa na kampuni ya Multi Choice.
AKA aliungana na mastaa hao katika moja ya hafla ya kukutana na
kusalimiana na mashabiki wa Afrika Kusini ambapo pia alitumbuiza. Rapper
huyo aliyefanya kazi na Diamond na Joh Makini alishare video
ikimuonesha akiongea na mastaa hao na kuwaeleza kuwa angependa pia
kuigiza kwenye tamthilia ya Empire.
Terrence anasikika akimueleza kuwa wataongeza na muongozaji, Lee Daniels ili amuongeze.
“Lucious & Cookie enjoyed the show. Maybe they’ll give me a role on
Empire. Tell Lee Daniels about the design,” aliandika AKA kwenye video
hiyo na kumtag Lee Daniels.
Taraji aliirepost video na kuandika: You were a wonderful host
@akaworldwide I AM A BIG FAN OF #AfricanMusic Thank you for being so
kind to us! AND YES WE SHOULD HAVE YOU ON THE SHOW @theoriginalbigdaddy.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment