Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani mkoani hapa .
Ofisa Habari wa timu hiyo,Saidi Karsandas alisema kuwa maandalizi ya kuelekea michezo hiyo kwao yanaendelea vizuri na Oljoro watatua jijini Tanga (leo)jana kwa ajili ya mechi hiyo ambayo ni muhimu kwa timu zote kujiandaa na michuano hiyo.
Karsandas alisema kikosi cha timu hiyo kinaendelea na mazoezi yake kwenye uwanja wa shule ya sekondari Usagara wakiwinda na mashindano ya ligi daraja la kwanza lengo likiwa kushiriki kwa mafanikio ili waweze
kupata nafasi ya kucheza ligi kuu msimu ujao.
Alisema baada ya kumalizika mechi hiyo watacheza na Panoni FC ya Kilimanjaro kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani kabla ya kuvaana na AfricanLyon ikiwa ni mechi ya ufunguzi wa michuano ya Ligi daraja la kwanza.
Akizungumzia hali ya kikosi hicho, Kocha Mkuu Ally Manyani alisema kuwa wachezaji wote wapo imara na hakuna majeruhi hata mmoja kitendo ambacho kinampa uhakika wa kuanza vema mashindano hayo.
Ofisa Habari hiyo alisema wanachama wa timu hiyo wanatarajia kuwa na kikao kitakachozungumzia masuala mbalimbali ya timu hiyo ikiwemo mkakati wao wa kuelekea michuano hayo
0 comments:
Post a Comment