WANAKIJIJI WAWILI KILINDI WANASHIKILIWA KWA MAUAJI ##


Wakazi  wawili wa kijiji cha Lomotio Wilayani hapa,wanashikiliwa na jeshi la polisi wakihusishwa na mauaji ya Kazenge Zakayo (20) aliyekufa kwa kuchomwa moto na kitu chenye ncha
kali.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga,Frasser Kashai alisema jana kuwa mauaji hayo yalifanyika  saa 1.00 jioni kijijini Lomotio kata ya Pagwi iliyopo tarafa ya Kwekivu.

Aliwataja wanaoshikiliwa na Polisi kuhusiana na tuhuma hizo kuwa ni Matatizo Mgongo (20) na Samwel Esay (22) ambaye ni mkulima kijijini hapo.

“Marehemu alikufa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali shingoni upande wa kushoto na watu wasiojulikana “alisema Kashai.

Alisema kufuatia mauaji hayo ,jeshi la Polisi linawashikilia watuhumiwa hao ili waweze kusaidia uchunguzi  na ili kuweza kuwanasa wengine zaidi.
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment