COASTAL UNION WANAENDELEA KUJIFUA KUELEKEA MCHEZO WAO NA NDANDA FC ##

TIMU ya Coastal Union ya Tanga leo imeendelea na mazoezi yake kwenye uwanja wa shule ya sekondari Popatlaly ikijiandaa na mechi yake dhidi ya Ndanda SC itakayochezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani wi kiendi hii.

Mazoezi hayo yaliyoanza saa kumi jioni na kumalizika saa kumi na mbili jioni yakisimamiwa na Kocha Mkuu Yusuph Chippo akiwa na Msaidizi wake,Benard Mwalala sambamba na Mkurugenzi wa Ufundi Mohamed Kampira.

Akizungumza mara baada ya kumalizika mazoezi hayo,Kocha Chippo amesema maandalizi ya kuelekea mechi hiyo yanaendelea vema na hakuna mchezaji hata mmoja ambaye ni majeruhi.

Chippo amesema kutokana na juhudi zinazofanywa na wachezaji kwenye mazoezi hayo wanamatumaini makubwa ya kuchukua pointi tatu muhimu kwenye mechi hiyo ambayo itakuwa ni ya kwanza kucheza nyumbani.
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment