MKAZI MMOJA WILAYA YA LUSHOTO STEPHAN JOSEPH AMEUAWA KIKATILI KWA KUCHOMWA KICHWANI NA KITU CHENYE NCHA KALI ##

Mkazi mmoja wa kijiji cha Shume B kata ya DOCHI wilaya ya lushoto STEPHAN JOSEPH mwenye umri wa miaka {38} ameuawa kikatili kwa kuchomwa kichwani  na kitu chenye ncha kali  na watu wasiojulikana.

Akiongea na waandishi wa habari kamanda wa jeshi la polisi mkoani tanga FRAISER KASHAI amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema mnamo tarehe 5/10/2014 majira ya saa nne kamili usiku mwili wa mkulima huyo ulikutwa kwenye shimo kandokando ya barabara ya mtae akiwa ameuawa.

KAMANDA WA JESHI LA POLISI MKOANI TANGA FRAISER KASHAI
Aidha mkuu huyo wa jesh ila polisi ametaja chanzo cha mauaji hayo kuwa hakijajulikana na hakuna mtu  aliyekamatwa kutokana na tukio hilo na msako mkali bado unaendelea ili kuwatia mbaroni wahalifu hao.
 
Hata hivyo kamanda kashai  amesema kuwa mwili wa marehemu umefanyiwa uchunguzi na madaktari na hatimaye kuukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu  kwa ajili ya mazishi.
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment