Tukio hilo lilitokea mara baada ya Mechi ambayo PSG iliifunga Bastia 2-0 Uwanjani Parc des Princes na Brandao akamsubiri Thiago Motta akipita kwenye Ukumbi kuelekea Vyumba vya Kubadili Jezi ndipo alipomtwanga Kichwa.
Kipigo hicho kilimsababisha Thiago Motta avunjike Pua na Uongozi wa Soka Nchini France uliamua kumfungia Miezi 6.
Kwa mujibu wa Gazeti Le Parisien Mwanasheria wa Brandao hatakata Rufaa kupinga Kifungo cha Mwezi mmoja Jela kwa vile wanategemea Adhabu hiyo itageuzwa na kuwa ya kutumikia Jamii bure kwa kipindi maalum.
Mahakamani, Brandao alikiri Kosa lake lakini alikataa kwamba alikusudia kutenda kosa hilo.
0 comments:
Post a Comment