Dawa
za antibiotics
Wagonjwa wanaotibiwa na dawa za viua vijasumu
ama antibiotics mara kwa mara huenda wakakabiliwa na hatari ya kupatwa na aina
ya pili ya ugonjwa wa kisukari ,watafiti wamegundua.
Utafiti uliochapishwa na Jarida la utafiti wa
damu ulifuatilia dawa zinazopewa mamilioni ya wagonjwa nchini Uingereza.
Waanzilishi wa utafiti huo wanasema kuwa
matokeo ya utafiti huo hayamaanishi kwamba dawa hizo husababisha kisukari ,na
badala yake maambukizi huenda ni ishara za mapema kwamba mtu anakabiliwa na
kisukari.
Wanasema kuwa kazi ya ziada inahitajika ili
kuelewa uhusiano huo.
antibiotics
''Ni utafiti mkubwa na wenye usaidizi
unaohusisha kisukari na utumiaji wa dawa za viuavijasumu miongoni mwa wakaazi
wa Uingereza,lakini kufikia sasa hatujui ni kipi kilichokuja mwanzo,ni kuku ama
ni mayai yake'',professa Jodi Lindsay wa chuo cha St Georges mjini London
alisema.
Utafiti huo uliangazia idadi ya dawa hizo
zilipewa wagonjwa 208,000 wa kisukari cha aina ya kwanza na ya pili mwaka mmoja
kabla ya kupatikana na ugonjwa huo ikilinganishwa na watu 816,000 wasio na
ugonjwa huo walio na umri sawa na jinsia sawa.
Karibia nusu ya wagonjwa hao walipewa dawa
hiyo wakati mmoja huku utafiti huo ukiendelea.
Watafiti walibaini kwamba hatari ya aina ya
pili ya kisukari ilipanda juu kutokana na idadi ya dawa za viuavijasumu
waliopewa.
0 comments:
Post a Comment