PICHA ZA MAELFU YA WAOMBOLEZAJI KUUAGA MWILI WA KAPTENI KOMBA ##


Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Kapteni John Komba,mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.Kapteni Komba anatarajiwa kuzikwa kijijini Kwake Litui wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma

 Jeneza lililobeba mwili wa marehemu Kapteni John Komba likiwa limebebwa kuelekea kwenye jukwaa maalum kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
 Familia ya Marehemu Kapteni John Komba ikiwa imesimama tayari kuupokea mwili wa marehemu kwenye viwanja vya Karimjee.
 Ni huzuni kubwa kwa familia ya marehemu.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiwa pamoja na Makamu wa Rais Ghalib Bilal (kushoto) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anna Makinda wakiwa kwenye viwanja vya Karimjee ambapo mwili wa Marehemu Kapteni John Komba uliagwa na Viongozi mbali mbali na wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akis
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akizungumza na   Makamu wa Rais Ghalib Bilal kwenye viwanja vya Karimjee ambapo mwili wa Kapteni John Komba ulikuwa unaagwa .
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye  akiimba wimbo maalum wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Kapteni John Komba aliyefariki tarehe 28 februari 2015 jijini Dar es Salaam.
 Viongozi wa CCM pamoja na wanamuziki wa muziki wa dansi wakiimba kwa pamoja nyimbo maalum wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Kapteni John Komba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoa heshima ya mwisho kwa marehemu Kapteni John Komba .
 Mzee Yusuf Makamba akifutmachozi wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Kapteni John Komba
 Kada wa CCM na Mwanasiasa mkongwe nchi Kingunge Ngombale Mwilu akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Kapteni John Komba
 Katibu wa NEC Idara ya Oganaizesheni CCM Dk. Mohamed Seif Khatib akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Kapteni John Komba
 Waziri wa Mambo ya Nje na uhusiano wa Kimataifa Bernad Membe akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Kapteni John Komba
 Viongozi na wananchi kutoka sehemu mbali mbali wakiwa kwenye foleni ya kwenda kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Kapteni John Komba kwenye viwanja vya Karimjee.
Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Arusha Mheshimiwa Catheline Magige akiondoka eneo la tukio baada ya kumaliza kutoa heshima zake za mwisho kwa marehemu Kapteni John Komba.

Jeneza lenye mwili wa aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM,Marehemu Kapteni John Komba likiwa kwenye viwanja vya Karimjee,jijini Dar es salaam,wakati wa shughuli ya kuaga.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Kapteni John Komba,mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.Kapteni Komba anatarajiwa kuzikwa kijijini Kwake Litui wilaya ya Nyasa Mkoani Ruvuma.
 Makamu wa Rais,Dkt. Mohamed Gharib Bilal na wake zake Mama Asha na Mama Zakhia wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Kapteni John Komba,mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
 Rais Mstaafu wa awamu ya pili,Alhaj Ali Hassa Mwinyi akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Kapteni John Komba,mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
 Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,Mh. Benjamin Mkapa na Mkewe Mama Anna Mkapa wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Kapteni John Komba,mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
 Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowassa na Mkewe Mama Regina Lowassa wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Kapteni John Komba,mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowassa akiifariji familia ya marehemu.
 Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania,Luteni Kanali Samuel Ndomba akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Kapteni John Komba,mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
 Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera na Uratibu wa Bunge,Mh. Jenista Mhagama akitoa heshima za mwisho akifuatana na Naibu IGP,Abdulrahman Kaniki.
 Kingunge Ngombale–Mwiru akitoa heshima za mwisho.
Kamanda Kova.
Baadhi wa Waheshimiwa Wabunge wakiifariji familia ya Marehemu.
Mhe. Ole Sendeka akibubujikwa na machozi kuondokewa na Mbunge mwenzake.
Familia ya Marehemu.
Watoto wa Marehemu Kapteni John Komba wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu baba yao.
Mjane wa Marehemu,Kapteni John Komba,Mama Salome Komba akiaga mwili wa mumewe
Khadija Kopa.
Umati wa viongozi mbali mbali pamoja na wananchi wakiwa kwenye viwanja vya Karimjee,jijini Dar es salaam wakati wa shughuli ya kuaga mwili wa marehemu Kapteni John Komba.

Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Sera na Uratibu wa Bunge,Mh. Jenista Mhagama akitoa salamu za Serikali wakati wa shughuli ya kuaga mwili wa marehemu Kapteni John Komba,mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii,Mh. Saidi Mtanda akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya Kamati yake.
Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki,Mh. Joshua Nassari akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akizungumza jambo na Mh. Joshua Nassari.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana akitoa salamu za Chama.
Mh. Muhongo akitoka kuaga mwili wa Kapteni Komba.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,Mh. Benjamin Mkapa akisungumza jambo na Katibu Mkuu wa CCM,Ndg. Abdulrahman Kinana.kushoto ni Spika wa Bunge,Mh. Anne Makinda.
Mama Regina Lowassa akizungumza jambo na Mama Sophia Kawawa.
Mh. Mkapa akizungumza jambo na Mh. Anne Makinda.




Mjane wa Marehemu.

































Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment