Stand
United imejiongeza kwakuibuka na pointi tatu baada ya kushinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Kagera
Sugar.
Mnigeria
Chidiebere maarufu kama Chidi ndiye amefunga mabao yote mawili.
Chidi
alifunga bao moja jana lakini mechi hiyo ikasimama katika dakika 80 kutokana na
mvua kubwa.
Mchezo huo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara ulianza jana na Stand United ikapata bao moja lililofungwa Chidiebele dakika ya 42. Chidiebele pia ndiye aliyeifungia Stand bao pekee ikiilaza Simba 1-0 wiki iliyopita.
Kwa matokeo hayo, Stand inatimiza pointi 21 baada ya kucheza mechi 17 na kusogea nafasi ya saba kwenye msimamo wa Ligi Kuu, ikiiteremsha Mtibwa Sugar nafasi ya nane.
0 comments:
Post a Comment