Chama cha riadha nchini Tanzania kimesema wanariadha wake wanaendelea vizuri na mazoezi chini ya kocha Francis John.
Kikosi cha wanariadha waliochaguliwa kinahusisha wale ambao walifanya vizuri dhidi ya Kenya katika mbio fupi (half marathon) za Kilimanjaro Marathon zilizofanyika Moshi, Kilimanjaro.
Kenya ilitawala katika mbio ndefu (full Marathon) kwa kushinda kumi bora zote katika mbio hizo za Kilimanjaro Marathon.
Wakimbiaji wanaofanya mazoezi Arusha ni Fabian Nelson na Bazi John kutoka chuo cha Polisi cha Moshi.
Wengine ni Alphonce Erick wa Arusha, Emmanuel Giniki na Joseph Theophil.
0 comments:
Post a Comment