YANGA YAZIDI KUTOA RAHA KWA RAIA WAKE GOLI 3 - 1 NDIZO ZILIZOPATIKANA KWENYE GEMU YA LEO ##

YANGA SC imezidi kuchanja mbuga kuelekea  kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kufuatia ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya JKT Ruvu, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam hii leo .

Kwenye Mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Yanga walitangulia kupata Bao la Kwanza kwa Penati iliyotolewa baada ya Amos Makwaya wa Ruvu JKT kulinawa shuti la Simon Msuva na Msuva mwenyewe kufunga Penati hiyo katika Dakika ya 35.

Bao la Pili la Yanga lilifungwa Dakika ya 42 na Danny Mrwanda baada ya kazi njema ya Mrisho Ngassa na Msuva.

Kwenye Dakika ya 44 Ruvu JKT walipata Bao lao moja Mfungaji akiwa Samuel Kamuntu mpaka timu zinakwenda  Mapumziko Yanga 2 Ruvu JKT 1.

Kipindi cha pili, Yanga SC walirejea na moto wao na kufanikiwa kupata bao la tatu lililofungwa na Msuva, tena akimalizia pasi ya Ngassa. Msuva sasa ndiye anaongoza kwa mabao Ligi Kuu, 11 dhidi ya 10 ya Kavumbangu.

Yanga SC waliendelea kutawala mchezo na kupeleka mashambulizi zaidi langoni mwa JKT, lakini hawakuwa na bahati ya mabao zaidi.


Kwa ushindi huo, Yanga SC inafikisha pointi 40 baada ya kucheza mechi 19, moja zaidi ya mabingwa watetezi, Azam FC wenye pointi 36.

Kikosi cha JKT Ruvu; Benjamin Haule, Damas Makwaya, Ramadhani Shamte, Renatus Morris, Mohammed Fakhi, Nashon Naftali, Amos Mgisa/Ally Bilal dk58, Jabir Aziz, Samuel Kamuntu, Iddi Mbaga/Emmanuel Pius dk41 na Alex
Abel.

Yanga SC; Ally Mustafa ‘Barthez’, Juma Abdul, Oscar Joshua, Mbuyu Twite, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Said Juma ‘Makapu’, Salume Telela, Haruna Niyonzima/Nizar Khalfan dk 87, Danny Mrwanda/Hussein Javu dk72, Mrisho Ngassa na Simon Msuva. 

LIGI KUU VODACOM

RATIBA

Jumamosi Aprili 4

Mtibw Sugar v Stand United

Coastal Union v Tanzania Prisons

Ruvu Shooting v Ruvu JKT

Ndanda FC v Mbeya City

Kagera Sugar v Simba (Mechi kuchezwa Kambarage, Shinyanga)
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment