
Mbwana Samata amewasili nchini
Ubelgiji na kusaini mkataba wa miaka minne na Club mpya ya FC Genk ili
kucheza katika ligi kuu ya nchi hiyo, Ubelgiji imekuwa moja ya nchi
zinazotoa wachezaji wakubwa ulaya na kikosi cha timu ya Taifa ya nchi
hiyo ni moja kati ya timu kali duniani.
Mbwana amesema katika ukurasa
wake wa Instagram kuwa anamshukuru Mungu kwa fursa hii na ataitumia
vyema ili kujiletea mafanikio na kuleta mafanikio kwa taifa lake pia.
Meneja wa mshambuliaji huyo, Jamal Kisongo, alisema amewasiliana na Samatta na kumweleza kwamba amefika salama na ameanza kufuata taratibu zote ili aweze kufanya kazi nchini humo.
Samatta ambaye alitwaa tuzo ya kuwa Mchezaji Bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani, alikubali kujiunga na timu ya KRC Genk na kugomea ofa zilizotolewa na klabu za Nantes na Olympique Marseille za Ufaransa
Meneja wa mshambuliaji huyo, Jamal Kisongo, alisema amewasiliana na Samatta na kumweleza kwamba amefika salama na ameanza kufuata taratibu zote ili aweze kufanya kazi nchini humo.
Samatta ambaye alitwaa tuzo ya kuwa Mchezaji Bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani, alikubali kujiunga na timu ya KRC Genk na kugomea ofa zilizotolewa na klabu za Nantes na Olympique Marseille za Ufaransa
0 comments:
Post a Comment