MBWANA SAMATA ASAINI MKATABA WA MIAKA MINNE KUCHEZEA TIMU YA GENK YA LIGI KUU UBELGIJI-{VIDEO} ##

SAM
Mbwana Samata amewasili nchini Ubelgiji na kusaini mkataba wa miaka minne na Club  mpya ya FC Genk ili kucheza katika ligi kuu ya nchi hiyo, Ubelgiji  imekuwa moja ya nchi zinazotoa wachezaji wakubwa  ulaya na kikosi cha timu ya Taifa ya nchi hiyo ni moja kati ya timu kali duniani.
Mbwana amesema katika ukurasa wake wa Instagram kuwa anamshukuru Mungu kwa fursa hii na ataitumia vyema ili kujiletea mafanikio na kuleta mafanikio kwa taifa lake pia.
Meneja wa mshambuliaji huyo, Jamal Kisongo, alisema amewasiliana na Samatta na kumweleza kwamba amefika salama na ameanza kufuata taratibu zote ili aweze kufanya kazi nchini humo.

Samatta ambaye alitwaa tuzo ya kuwa Mchezaji Bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani, alikubali kujiunga na timu ya KRC Genk na kugomea ofa zilizotolewa na klabu za Nantes na Olympique Marseille za Ufaransa
SAM2
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment