Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, akiwasilisha mbele ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, taarifa yake kuhusu ziara yake aliyoifanya hivi karibuni nchi Burundi. Katika taarifa yake ameelezea kutiwa matumaini na uteuzi wa Rais Mstaafu Mhe. Benjamin Mkapa kuwa Mwezeshaji wa majadiliano ya kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi.
Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akizungumza kwa niaba ya Jumuiya ya Afrika Mashariki katika mkutano wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa lililokutana Ijumaa uliojadili kuhusu Burundi. Aliyeketi nyuma ya Balozi, ni Bw. Khamis Abdallah Afisa wa Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Burundi, Bw. Alain Amic Nyamitwe naye akielezea hali ya mambo na jitihada mbalimbali ambazo serikali ya Burudi imekuwa ikichukua katika kurejesha hali ya amani na utulivu.
Wajumbe wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, katika mkutano wao wa Ijumaa ambapo baada ya kupokea taarifa kuhusu Burundi, waliendelea na kikao chao cha ndani.
0 comments:
Post a Comment