DOMAYO WA AZAM ATAANZA KUJIFUA OCTOBA 1 BAADA YA KUMALIZA MUDA WA MAPUMZIKO KUFUATIA KUFANYIWA UPASUAJI WA NYAMA ZA PAJA ##

 KIUNGO Frank Domayo  wa azam fc ataanza mazoezi mepesi Oktoba 1, mwaka huu baada ya kumaliza muda wa mapumziko kufuatia kufanyiwa upasuaji wa nyama za paja.
 
Domayo aligundulika kuchanika vibaya nyama za paja, baada tu ya kusajiliwa na Azam FC Juni mwaka huu, kufuatia kumaliza Mkataba wake wa miaka miwili Yanga SC.

Kufuatia hali hiyo, alipelekwa Afrika Kusini alikofanyiwa opersheni na kutakiwa kupumzika kwa miezi mitatu- na sasa yuko tayari kuanza jaribio la kurejea uwanjani.

Aidha, winga Joseph Kimwaga akiyekwenda kufanyiwa upasuaji pamoja na Domayo, naye ameanza mazoezi mepesi tangu mwishoni mwa wiki.
Kimwaga aliumia goti mwaka jana katika mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu baada ya kuibuka vizuri kikosi cha kwanza cha Azam kufuatia kupandishwa kutoka akademi.

Amekuwa nje kwa muda wote akijaribu kutibiwa hapa nyumbani bila mafanikio kabla ya kupelekwa Afrika Kusini, naye sasa anajaribu kurudi tena uwanjani.
Umaarufu wa Kimwaga ulikuja baada ya kuifungia Azam FC bao la tatu katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Yanga SC katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu uliopita.
 
Kwa upande mwingine, mshambuliaji John Raphael Bocco aliyeumia katika Robo Fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati dhidi ya El Merreikh ya Sudan mwezi uliopita, naye anatarajiwa kuanza mazoezi mapema wiki ijayo.

Tayari majeruhi mwingine wa muda mrefu wa Azam FC, Waziri Salum ameanza mazoezi tangu mwishoni mwa wiki.     
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment