PAUL SCHOLES AMETOBOA JINSI SIR ALEX FERGUSON ALIVYOKUWA AKIPANGA MIKAKATI YA KILA MECHI ZA MANCHESTER UNITED ##

PAUL SCHOLES ametoboa jinsi Sir Alex Ferguson alivyokuwa akipanga mikakati ya kila Mechi za Manchester United wanazokabiliana nazo na kusema hata Mechi ndogo yeye alizichukulia kama ‘Fainali ya Kombe la Dunia.’

Scholes, ambae sasa amestaafu kucheza Soka baada ya kuitumikia Man United katika maisha yake yote ya Soka na kucheza Mechi 499 chini ya Sir Alex Ferguson, amesema Ferguson alijua mno namna ya kuongea na kuhamasisha.

Scholes amesema: “Siku za Mechi Uwanjani Old Trafford tulifika Saa 6 na nusu Mchana na Sir Alex alionana na kila Mchezaji mmoja mmoja Ofisini kwake. Mara nyingine alikwambia huchezi Mechi hiyo na mara nyingine alikuelekeza nini anataka ufanye katika Mechi hiyo.”

Baada ya hapo Kikosi kizima kilijumuika kwa Mkutano wa pamoja ambao pia ulipitia kuchambua Video za Wapinzani wao wa Siku hiyo kwa Muda wa Dakika 10.

Scholes ameeleza: “Sir Alex alikuwa na uwezo wa kuzifanya Mechi ndogo, kama zile za Raundi ya mwanzo za FA CUP na zile dhidi ya Timu za chini za Ligi zionekane kama ni Fainali ya Kombe la Dunia!”
Aliongeza: “Mazungumzo yake yanakuingia kichwani na kukuhamasisha!”

Hata hivyo, Scholes alibainisha si mara zote Ferguson alikuwa akifanya matayarisho kwa aina hiyo kwani kuna wakati alikuja na kutamka Sentensi moja tu.

Scholes amesema: “Mara chache, si Mechi kubwa, tulikuwa tukimngoja na anaingia akionekana na hasira. Halafu hutoa amri: ‘Nendeni mkaifunge Timu hii! Sentensi moja tu na huyo katoka!”
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment