TIMU YA STAND UNITED IMESEMA KUWA INAKIBARUA KIGUMU DHIDI YA MGAMBO SHOOTING ##

TIMU ya Stand United imesema kuwa inakibarua kigumu dhidi ya Mgambo Shooting ikiwa ni mechi yao ya Ligi kuu soka Tanzania bara lengo kuweza kupata ushindi ili kutimiza ahadi waliomuhaidi Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga ,Ally Lufungu kupata matokeo mazuri kila mchezo.

Hivyo timu hiyo italazimika kuingia uwanjani hapo kama Simba aliyejeruhiwa ili kuhakikisha inapata matokeo mazuri kwao ndani ya dakika 90 za mchezo huo.

Hayo yalisemwa leo na Mkurugenzi wa Benchi la Ufundi la timu hiyo,Muhibu Kanu ambapo alisema kuwa timu hiyo ina deni ambalo linapaswa kufanyiwa kazi ipasavyo kwenye mechi yao hiyo ya leo ili waweze kutimiza matakwa yao.

Akizungumzia maandalizi ya timu hiyo,Kanu amesema kuwa kikosi chao kipo imara kwa ajili ya kufanya vizuri ili kuweza kusongea kwenye nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi hiyo kutokana na mapungufu walioyafanyia kazi kwenye mechi yao iliyopita dhidi ya Nanda FC na kukubali kichapo cha bao 4-1.

Amesema kuwa kwenye mchezo huo wachezaji wao watano waliokosa mchezo huo ambao walikuwa majeruhi tayari walikwisha kupona na wapo imara kuweza kucheza kwenye mechi hiyo ya leo.

Amewataja wachezaji hao ambao hawakuonekana kwenye mchezo wao uliopita na wapo tayari kupambana kuhakikisha ushindi unapatikana kuwa ni Mohamed Soudy,Iddy Moby,Roberty Magadula,Mohamed Jingo na Hamadi Juma (ambaye alikuwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya vijana ya Tanzania).

   “Kama ujuavyo sisi tunapaswa kupambana vilivyo ili kuweza kupata matokeo mazuri kwa sababu mechi yetu ya kwanza tulipoteza mchezo huo hivyo ni lazima kushinda kwani tunakumbuka sana kauli ya tuliomuhaidi pia Mbunge wetu Steven Masele kushinda mechi za nyumbani na ugenini “Amesema Kanu.

Stand United ilishafika mkoani lakini ikaamua kujichimbia wilayani Korogwe Kabla ya kutua jijini Tanga jana jioni kwa ajili ya mazoezi kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani.

Wakati huo huo,Kocha Mkuu wa timu ya Mgambo Shooting,Bakari Shime amesema kuwa wimbi uliotumika kuwakata Kagera Sugar kwenye mechi ya Ufunguzi wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara ndio atakaoutumia kwenye mechi hiyo.

Shime ameyasema hayo mara baada ya kumalizika mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea kwenye viwanja vya Kange Jeshini jijini hapa ambapo alisema wao wamejipanga vilivyo wanashinda mechi zote zilizopo mbele yao.

Akizungumza hali ya wachezaji,Kocha Shime amesema kuwa kikosi chake kipo vizuri na hakuna majeruhi wa aina yoyote na kuwahaidi ushindi wapenzi na mashabiki wake.

Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment