YANGA SC YAFANYA KWELI DSM 2-1 USHINDI WA KWANZA LIGI KUU ::##

YANGA SC imefanya kali yake leo baada ya  ushindi wa kwanza katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuichapa  Prisons ya Mbeya mabao 2-1 .

Mbrazil Andrey Coutinho alikuwa wa kwanza kuipatia Yanga SC bao dakika ya 34 Kwa ujumla, Yanga SC inayofundishwa na Mbrazil Marcio Maximo, ilicheza vizuri kipindi cha kwanza, wakati Prisons pamoja na kuonyesha upinzani, lakini ilioneiana kuzidiwa. 

Prisons ilikwenda mapumziko  ikiwa pungufu, baada ya beki wake, Jacob Mwakalobo kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 39 baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano na refa Andrew Shamba wa Pwani, kufuatia kumchezea vibaya Ngassa.

Kipindi cha pili, Prisons  wakasawazisha dakika ya 67, mfungaji Ibrahim Kahaka aliyetokea benchi ambaye alimalizia pasi ya Jeremiah Juma.

Dakika mbili baadaye, Simon Msuva aliifungia Yanga SC bao la ushindi akimalizia krosi maridadi ya Ngassa .

WACHEZAJI WA YANGA : ; Deo Munishi ‘Dida’, Juma Abdul, Edrwad Charles, Kevin Yondan/Rajab Zahir dk77, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima, Hassan Dilunga/Hamisi Thabit dk54, Genilson Santana ‘Jaja’, Mrisho Ngassa na Andrey Coutinho/Simon Msuva dk58. 


  WACHEZAJI WA PRISONS: Mohamed Omar, Salum Lameya, Laurian Mpalile/Boniface Hau dk74, Nurdin Chona, Lugano Mwangama, Jumanne Elfadhil, Meshack Olest/Julius kwangwa dk35, Freddy Dungu, Jacob Mwakalobo, Amin Omary/Ibrahim Kahaka dk53 na Jeremiah Juma.
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment