CAF CHAMPIONZ LIGI TP MAZEMBE HOI BAADA YA KUZIDIWA KWA BAO ZA UGENINI ##

Klabu ya Congo DR, AS Vita, Jana imeifunga Klabu ya Tunisia Bao 2-1 katika Mechi ya Marudiano ya Nusu Fainali ya CAF CHAMPIONZ LIGI iliyochezwa huko Tunis, Tunisia na sasa wametinga Fainali kwa Jumla ya Bao 4-2 baada kushinda Mechi ya Kwanza pia 2-1.

Hii ni mara ya kwanza kwa AS Vita kufika Fainali na watacheza  na ES Setif ambapo imeibuka kidedea  huko Lubumbashi.

Klabu ya Congo DR, TP Mazembe, Leo Uwanjani kwao Stade TP Mazembe Lubumbashi imeifunga Entente Sportive de Sétif  ya Algeria Bao 3-2 katika Mechi ya Marudiano ya Nusu Fainali ya CAF CHAMPIONZ LIGI lakini imetupwa nje kwa Bao za Ugenini

Katika Mechi ya Kwanza, ES Setif iliifunga TP Mazembe Bao 2-1 na hivyo Jumla ya Magoli kwa Mechi mbili kuwa 4-4 na Setif kutinga Fainali kwa ubora wa Bao za Ugenini.

Kwenye Fainali, ES Setif watacheza na Klabu nyingine ya Congo DR, AS Vita, ambao Jana waliifunga Club Sportif Sfaxien ya Tunisia Bao 2-1 na pia kushinda Mechi ya kwanza kwa Bao hizo hizo.

Hadi Mapumziko TP Mazembe walikuwa mbele kwa Bao 2-1 kwa Bao za Daniel Nii Adjei
na Coulibaly na Setif kufunga Bao lao kupitia Abdelmalek Ziaya.

Kipindi cha Pili, Bolingi aliipa TP Mazembe Bao la 3 na hadi hapo Klabu hiyo ya Lubumbashi ilikuwa ipo Fainali lakini Dakika ya 75 Younes Sofiane aliwakata maini kwa kuifungia Setif Bao la Pili.
Hadi mwisho TP Mazembe 3 ES Setif 2.

Fainali ya CAF CHAMPIONZ LIGI  itachezwa kwa Mechi mbili, Nyumbani na Ugenini, hapo Wikiendi ya Oktoba 25 na Marudiano Novemba 1.

FAINALI

AS VITA V ES SETIF
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment