Timu inayoiwakilisha tanga kwa uzuri kwa upande wa ligi kuu ya vodacom Tanzania coastal union leo imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya panoni fc ya kilimanjaro.
Katika mchezo wa leo ulionekana kuwa na ushindani wa hali ya juu kwa vipindi vyote vuta ni kuvute kwa kila lango coastal walitumia uthaifu wa mabeki wa panoni na kufanikiwa kuweka wavuni goli mbili kabla ya dakika 90 kuamua yake.
Mchezo huu wa siku ya leo ulikuwa ni wa kujipima nguvu uliochezwa uwanja wa mkwakwani huku mabao ya coastal union yalifungwa na keneth masumbuko na omary mahamud na la kufutia machozi kwa upande wa panoni fc lilifungwa na laurance mbawa
0 comments:
Post a Comment