COASTAL UNION YAAHIDI KUZINGANGANIA POINT TATU KWA FUJO KUTOKA KWA NDUGU ZAO WA MJI MMOJA MGAMBO SHOOTING ##

TIMU ya Coastal Union imeendelea kujimarisha katika maandalizi ya kuelekea mechi yao na Mgambo Shooting inayotarajiwa kuchezwa kesho kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani ikiwa ni muendelezo wa Ligi kuu soka Tanzania bara.

Coastal Union imekuwa ikifanya mazoezi mara moja kila siku kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlaly ikijiwinda na mechi zake za Ligi hiyo ambayo msimu huu inaonekana itakuwa na upinzani mkubwa.


Kocha Mkuu wa Coastal Union amesema  kuwa kikosi chake kimeimarika vilivyo ili kuweza kuhakikisha wanapata pointi tatu muhimu kila mchezo lengo likiwa kumaliza ligi mzunguko wa kwanza wakiwa kwenye nafasi za juu.


Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment