MKUCHIKA AMEWAAGIZA MAAFISA TAKUKURU KWENYE HALMASHAURI NCHINI KUHAKIKISHA WANAKWENDA KUKAGUA TAARIFA YA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO ##



WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora,George Mkuchika amewaagiza maafisa Takukuru kwenye Halmashauri nchini  kuhakikisha wanakwenda kukagua taarifa ya  fedha za miradi ya maendeleo jinsi  zilivyotumika kwenye maeneo yaliyokusudiwa ili kuweza kubaini hali halisi.

Hayo aliyasema wakati akizungumza kwenye kikao cha Ushauri wa Mkoa wa Tanga (RCC) ambapo alisema kuwa miradi mingi kwenye halmashauri hapa nchini imegauzwa kuwa sehemu za kuchukulia fedha kwa watumishi wasiokuwa waaminifu jambo ambalo linakwamisha shughuli za maendeleo.


Alisema kuwa jambo hilo linatokana na wasimamizi wakuu wa halmashauri wakiwemo wakurugenzi wa Halmashauri na wataalamu wanachangia kwa asilimia kubwa kushindwa kusimamia miradi ya maendeleo inayoendeshwa kwenye maeneo yao hali inayopelekea kujengwa chini ya kiwango na kushindwa kudumu kwa muda mrefu.

   “Kwenye suala hili hakuna jinsi lazima maafisa Takukuru kwenye halmashauri kuacha kukaa ofisini badala yake mhakikisha mnakwenda kuziangalia fedha za miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye maeneo yenu kubaini mambo yanayokwenda nah ii itasaidia uwajibikaji kwa wahusika “Alisema Mkuchika.


Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment