WATU WAWILI WAMEKAMATWA NA MILIPUKO NANE YA MIAMBA #NA MKULIMA MOJA AKUTWA NA RISASI 39##


Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga linawashikilia raia wawili wa kigeni kutoka nchini Nigeria kwa tuhuma za kukutwa wakiwa na milipuko nane ya miamba ya madini pamoja na waya wa kuunganisha milipuko hiyo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga,Fresser Kashai alithibitisha kutoka tukio hilo ambapo alisema lilitokea Octoba 12 mwaka huu saa sana mchana huko Kijiji cha Kigwashi Kata ya Mashewa Tarafa ya Magoma wilayani Korogwe .

Aliwataja raia hao wa kigeni waliokamatwa kuwa ni Keneth Ekenee (31) na Ameki Boniface(31) wakiwa nyumbani kwa mwenyeji wao Frank alimaarufu Miki ambaye baada ya tukio hilo alikimbia akiwaacha wenyeji wake wakiwa hawajui pa kwenda.
Kwa upande mwingine Mkulima mmoja na mkazi wa Morogoro Michael Charles(28)amekamatwa na Polisi kwa tuhuma za kukutwa na risasi 39 alizokuwa akizisafirisha bila kuwa na kibali halali jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga Frasser Kashai alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Oktoba 8 mwaka huu majira ya saa 5.00 asubuhi huko katika eneo la Maili kumi Kata ya Segera wilayani Korogwe akiwa katika basi lenye namba za usajili T510 CLB aina ya Nissan Caravan akitokea Monduli mkoani Arusha kuelekea Morogoro.

Aidha watuhumiwa wote  wanatarajiwa kufikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment