Watanzania
wanatakiwa kupigia kura jezi ya timu ya Taifa ya nyumbani na ugenini
kupitia mtandao wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wa www.tff.or.tz ambapo jezi hizo zimewekwa.
TFF
ilipokea mapendekezo ya mwonekano mpya wa jezi ya timu ya Taifa kutoka
kwa Watanzania 86. Jezi 11 za nyumbani, bukta nane za nyumbani, jezi
nane za ugenini na bukta tano za ugenini ndizo zimepitishwa kwa ajili ya
kupigiwa kura.
Mwisho
wa kupiga kura ni Desemba 31 mwaka huu. Mpigaji kura anatakiwa
kubonyeza kwenye jezi na bukta ambayo ameichagua. Anatakiwa kufanya
hivyo kwa jezi ya nyumbani na jezi ya ugenini.
Tunawashukuru wote waliojitokeza kupendekeza mwonekano mpya wa jezi ya timu ya Taifa.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment