NAIBU WAZIRI MH.UMMY MWALIMU AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MAZINGIRA MKOANI MTWARA ##

Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb) Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais alifanya ziara ya kukagua Mazingira Mkoani Mtwara hususani katika eneo la Mdenga, Manispaa ya Mtwara.

Chimbuko la ziara hii ni malalamiko yaliyotolewa na wananchi kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Abdulrahman Kinana alipokuwa kwenye ziara ya kikazi mkoani humo


Afisa Uhusiano wa kampuni ya SBS, Bw. Geofrey Kanenge  (katikati) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Ummy Mwalimu (Mb) (wa pili kushoto)  kuhusu udhibiti wa utiririshaji wa maji taka yatokanayo na usafishaji wa mapipa yenye kemikali unavyofanywa na kampuni hiyo wakati wa ziara ya ukaguzi wa mazingira mkoani Mtwara.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Ummy Mwalimu (katikati) akipata maelezo kuhusu ubanguaji wa korosho kutoka kwa Uongozi wa Kiwanda cha Micronix  kilichopo mkoani Mtwara wakati wa ziara aliyoifanya mkoani humo.
Sehemu ya Wananchi wakimsikiliza Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mheshimiwa Ummy Mwalimu (hayupo pichani) wakati wa ziara ya kukagua hali ya Mazingira ya viwanda  aliyoifanya mkoani Mtwara

Eneo la bwawa la asili la Mdenga lililofukiwa kinyume cha sheria na kampuni ya SBS inayojishughulisha na urejelezaji wa taka mkoani Mtwara na kusababisha uharibifu wa mazingira katika eneo hilo.
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment