Humud
ambaye aliwahi kuzichezea klabu mbalimbali hapa nchini ikiwemo Simba
amehaidi kufanya makubwa kwenye kikosi cha wagosi wa kaya mambacho
kinajiwinda na michuano ya Ligi kuu soka Tanzania bara.
Beki
huyo machachari ambaye aliondoka Simba baada ya kufungwa na Yanga
kutokana na kutokea migogoro akaamua kwenye kujiunga na Sofa Paka
ya nchini Kenya.
Akizungumza
na waandishi wa Habari jana,Ofisa Habari wa Coastal Union,Oscar
Assenga amesema kuwa wanamatumaini makubwa na mchezaji huyo
ambaye alikuwa tishio kwenye vilabu mbalimbali hapa nchini alivyowahi
kuvichezea.
“Sasa tumeanza kufanya mabadiliko bado mambo yatakapo kuwa mazuri zaidi
tutawajulisha nini tumekifanya tena kwenye kikosi chetu “Amesema Assenga.
Hudumu
tayari alishatua jijini Tanga na ameungana na wachezaji wenzake kwenye
mazoezi yanayoendelea kwenye viwanja wa Disuza jijini Tanga chini
ya Mkurugenzi wa Benchi la Ufundi la Coastal Union Mohamed
Kampira.
Wachezaji
wengine waliosajiliwa kwenye kipindi cha dirisha dogo na Coastal
Union ni wachezaji wa kati ambao ni Bakari Sadiq aliyekuwa nchini
Denmark na sasa alikuwa akiichezea klabu ya Friends Rangers ya
Dar es
Salaam.
Hata
kadhalika na Godfrey Wambura ambaye alikuwa ni mchezaji wa Kagera Sugar
aliyekataa kwenda Simba msimu huu ikashindikana sasa ametua Coastal
Union.
Kwa
upande wake,Humud amesema amejisikia faraja kubwa sana kusajiliwa na
Coastal Union na kuhaidi kushirikiana na wachezaji wengine ili kuweza
kuipa mafanikio timu hiyo.
0 comments:
Post a Comment