CHIDI BENZ AOKOKA HUKUMU YA KIFUNGO CHA MIAKA MIWILI JELA BAADA YA KULIPA FAINI ##


Hakimu wa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, leo ametoa hukumu ya kifungo cha miaka miwili jela au kulipa faini kwa rapper, Chidi Benz.

Chidi alipandishwa kizimbani mahakamani hapo kusomewa mashtaka matatu ya kukutwa na madawa ya kulevya mwaka jana. 

Alikuwa nje kwa dhamana ya shilingi milioni 1 pamoja na wadhamini wawili wasiokuwa na hatia. Faini anayotakiwa kulipa ni shilingi laki tisa.

Rashid Abdallah Makwaya 'Chiddy Benzi' amehukumiwa kifungo cha miaka mwili jela au kulipa faini ya Sh 900,000, baada ya kutiwa hatiani kwa makosa matatu, ikiwemo kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroin zenye thamani ya Sh. 38,638, bangi ya Sh. 1,720 na vifaa ya kuvutia dawa hizo kijiko na kigae. 

Tukio hilo lilitokea October 25 mwaka jana katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam akiwa anaelekea jijini Mbeya kwenye show.

Hata hivyo, mwimbaji huyo wa wimbo Dar es Salaam Stand Up, ameachiwa  huru baada ya kulipa faini hiyo ya Sh. 900,000 na amerejea nyumbani kwao Ilala kuendelea na maisha ya uraiani. 
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment