TANZANIA YAICHAPA 5-3 KENYA KWENYE BEACH SOCCER. ##
















Timu ya Taifa ya Tanzania ya Mpira wa Miguu wa Ufukweni (Beach  Soccer) jana imeibuka na ushindi wa mabao 5- 3 ugenini dhidi wa wenyeji timu ya Taifa ya Kenya kwenye mchezo uliofanyika kwenye  Uwanja wa fukwe za Hotel ya Big Tree Pirates jijini Mombasa. 




Katika mchezo huo mabao ya Tanzania yalifungwa na Ali Rabbi mabao manne  na Mwalimu Akida bao moja .

Kipindi cha kwanza kilimazika kwa Tanzania kupata mabao 2 Kenya 1,  kipindi cha pili kilimalizika Tanzania 4 Kenya 3 na kipindi cha  tatu na cha mwishokwa mchezo kimalizika kwa Tanzania kupata mabao  5 Kenya 3.

Mechi ya marudiano inatarajiwa kuchezwa jumamosi wiki hii Februari  21, 2015 jijini Dar es salaam, na endapo timu ya Taifa ya Tanzania  itafanikiwa kuwatoa Kenya, itacheza na timu ya Taifa ya Misri  katika hatua inayofuata.
Mchezo wa kwanza utafanyika kati ya tarehe 7,8 Machi 2015 jiji Dar  es salaam na marudiano yatafanyika nchini Misri kati ya tarehe  13,14 Machi 2015.

 Timu inarejea leo jijini Dar es salaam majira ya saa 11 jioni  ikitokea jijini Mombasa nchini Kenya.

 IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment