NKURUNZIZA AONYA KUHUSU AL SHAABAB ##

Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi amejitokeza kwa mara ya kwanza tangu jaribio la mapinduzi la jumatano iliyopita.

Rais Nkurunziza akihutubia waandishi wa habari katika ikulu ya Bujumbura alionya kuwa kuna tishio la shambulizi la kigaidi kutoka kwa kundi la waislamu kutoka Somalia wenye uhusiano na Al-Qaeda , Al Shabaab.

Aliwaambia wandishi wa habari wa kimataifa kuwa tishio hilo la mashambulizi sio tu kwa taifa lake bali pia kwa Kenya na Uganda .

Wapinzani wake wanashuku ni njama ya kuidhinisha makabiliano makali na waandamani hapo kesho

 Hata hivyo mwaandishi wa BBC aliyeko Bujumbura an asema kuwa Nkurunziza hakuzungumzia lolote kuhusu hali ilivyo nchini Burundi wala tishio la mapinduzi dhidi yake.

Aliondoka ghafla akiwa mongoni mwa msafara uliolindwa kikamilifu.

Wapinzani wake hata hivyo wanasema huenda hiyo ni njama ya rais Nkurunziza kuidhinisha makabiliano makali dhidi ya wapinzani wake ambao tayari wameagiza wafuasi wao kujitokeza kwa wingi hapo kesho kuendelea na maandamano ya kumtaka asiwanie kipindi cha tatu katika kura za urais zitakazofanyika mwezi ujao.

Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment