Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi amejitokeza kwa mara ya kwanza tangu jaribio la mapinduzi la jumatano iliyopita.
Rais
Nkurunziza akihutubia waandishi wa habari katika ikulu ya Bujumbura
alionya kuwa kuna tishio la shambulizi la kigaidi kutoka kwa kundi la
waislamu kutoka Somalia wenye uhusiano na Al-Qaeda , Al Shabaab.
Aliwaambia
wandishi wa habari wa kimataifa kuwa tishio hilo la mashambulizi sio tu
kwa taifa lake bali pia kwa Kenya na Uganda .
Wapinzani wake wanashuku ni njama ya kuidhinisha makabiliano makali na waandamani hapo kesho
Hata hivyo mwaandishi wa BBC
aliyeko Bujumbura an asema kuwa Nkurunziza hakuzungumzia lolote kuhusu
hali ilivyo nchini Burundi wala tishio la mapinduzi dhidi yake.
Aliondoka ghafla akiwa mongoni mwa msafara uliolindwa kikamilifu.
Wapinzani
wake hata hivyo wanasema huenda hiyo ni njama ya rais Nkurunziza
kuidhinisha makabiliano makali dhidi ya wapinzani wake ambao tayari
wameagiza wafuasi wao kujitokeza kwa wingi hapo kesho kuendelea na
maandamano ya kumtaka asiwanie kipindi cha tatu katika kura za urais
zitakazofanyika mwezi ujao.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments:
Post a Comment