SERENA AMKEMEA MWANDALIZI WA INDIAN WELLS

Image copyrightGetty
Image captionSerena Williams na Angelique Kerber
Mchezaji anayeorodheshwa wa kwanza duniani katika tenisi ya wanawake Serena Williams ameshtumu matamshi ya mwandalizi mmoja wa mchezo huo kwamba wachezaji wanawake katika mecho huo wanawategemea sana wanaume.
Raymond Moore aliwaambia waandishi kabla ya siku ya fainali huko India Wells kwamba wanawake wanafaa kupiga magoti na kumshukuru mungu kwa wachezaji kama vile Roger Federer na Rafael Nadal kuwa waliubeba mchezo huo.
Williams alisema matamshi yake yanawatusi wanawake ambao hawana haja ya kumpigia magoti mtu yeyote.
Image copyrightAP
Image captionSerna Williams
Bwana Moore ambaye pia alizungumzia kuhusu maumbile ya kuvutia ya baadhi ya wachezaji wanawake ameomba msamaha kwa matamshi yake.
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment