TENISI: DJOKOVIC ATAKA WANAUME WALIPWE ZAIDI

Image copyrightEPA
Image captionNovak Djokovic
Mchezaji nambari moja duniani katika mchezo wa tenisi Novak Djokovic amekosoa kutolewa kwa kiasi cha fedha sawa miongoni mwa wanaume na wanawake katika mchezo huo,akisema wanaume wanafaa kulipwa zaidi kwa kuwa wana mashabiki wengi.
Baada ya kushinda taji la BNP Paribas huko India Wells,alitetea kiwango cha mashabiki kuangazia kiwango cha fedha kinachotolewa kwa wanamichezo wa jinsia zote mbili.
Awali,mkurugenzi mkuu wa mashindano ya Indian Wells Ray Moore alisema kuwa michuano ya WTA inafanikishwa kutokana na kiwango cha mashabiki wanaowashabikia wachezaji wa kiume.
Image copyrightAFP
Image captionSerena Williams
Djokovic aliyataja matamshi yake kama yasio sawa.
Mchezaji huyo wa Serbia alisema kuwa wanawake walipiginia walichokuwa wakitaka na wakapata,na kwamba wachezaji wanaume wanafaa kupigania haki zao zaidi.
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment