Utawala nchini Niger umetangaza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kwa wanajeshi waliouawa na wapiganaji wa kundi la Boko Haram kwenye mji wa Bosso ulio karibu na mpaka kati ya nchi hiyo na Nigeria.
Wanajeshi 26 kutoka Niger na mafisa wawili kutoka Nigeria waliuawa wakati wa shambulizi hilo la siku ya Ijumaa.
Zaidi ya wanajeshi 100 pamoja na raia pia walijeruhiwa.
Karibu wapiganaji 58 wa Boko Haram nao waliuawa wakati walijaribu kuuteka mji wa Bosso.
0 comments:
Post a Comment