MECHI ZIJAZO KWA UPANDE WA UEFA CHAMPION LIGI JUMANNE NA JUMATANO KWA UPANDE WA RAUNDI YA PILI MECHI ZA MAKUNDI ##




 JUMANNE SEPTEMBER  30

KUNDI E

PFC CSKA Moskva v FC Bayern München
-Mwaka Jana, CSKA walitolewa na Bayern kwa kuchapwa 3-1 kwao Moscow baada kupigwa 3-0 huko Munich.

Manchester City FC v AS Roma
-Mara ya mwisho kwa Man City kuifunga Klabu ya Italy ni Msimu wa 1978/79 walipoichapa 3-0 AC Milan kwenye Raundi ya Tatu ya UEFA Cup na kuibwaga nje kwa Jumla ya Bao 5-2 kwa Mechi mbili.

KUNDI F

APOEL FC v AFC Ajax

-Ajax hawajashinda Ugenini katika Mechi 7 za UEFA CHAMPIONZ LIGI na mara ya mwisho kushinda ni Oktoba 2011 walipoichapa GNK Dinamo Zagreb Bao 2-0.

Paris Saint-Germain v FC Barcelona

-Klabu hizi zina uhusiano kwa baadhi ya Watu wake wa sasa kwani Makocha Laurent Blanc wa PSG na Luis Enrique wa Barcelona walicheza pamoja huko Nou Camp kwenye Msimu wa 1996/97.

Nae Staa wa PSG, Zlatan Ibrahimović, alikuwa huko Barca Msimu wa 2009/10 na kutwaa Vikombe Vinne na kufunga Bao 16 katika Mechi 29 za La Liga.

Nao Thiago Motta na Maxwell, wote wa PSG, wameshawahi kuichezea Barca.

KUNDI G
Sporting Clube de Portugal v Chelsea FC
-Sporting wameshinda Mechi zao 3 zilizopita za Nyumbani dhidi ya Klabu za England bila kufungwa hata Bao na kipigo chao pekee ni Msimu wa 2007/08 kwenye Mechi ya Kundi la UCL walipofungwa 1-0 na Manchester United.

FC Schalke 04 v NK Maribor

-Maribor hawajawahi kuifunga Klabu yeyote kutoka Germany katika Mechi 4 za Mashindano ya Ulaya.

KUNDI H


FC Shakhtar Donetsk v FC Porto
-Porto, kwenye Mechi ya Kundi ya Msimu wa 2011/12 waliifunga Shakhtar huko Ukraine Bao 2-1 kufuatia ushindi wao wa Nyumbani wa 2-1.

FC BATE Borisov v Athletic Club

-BATE, ambao wamefungwa Mechi zao zote 8 dhidi ya Klabu za Spain kwenye Mashindano ya Ulaya, watacheza Mechi hii kwa mara ya kwanza Mjini kwao Donetsk baada ya Mechi zao 9 zilizopita ambazo walikuwa wakiutumia Mji wa Minsk.

Jumatano Oktoba 1

KUNDI A

Club Atlético de Madrid v Juventus

-Atlético walishinda Mechi 5 kati ya 6 walizocheza Nyumbani za UCL Msimu uliopita na wameshinda Mechi 17 kati ya 19 zilizopita walizocheza Uwanjani kwao Vicente Calderón kwenye Mashindano ya UEFA.

Malmö FF v Olympiacos FC

-Hii ni Mechi ya kwanza kwa Malmö kucheza Nyumbani kwenye UCL na hii ni mara ya kwanza kukutana na Klabu kutoka Ugiriki.

KUNDI B

PFC Ludogorets Razgrad v Real Madrid CF

-Msimu uliopita, Real Madrid, kwenye UCL, walifunga Jumla ya Bao 20 katika Mechi 6 za Ugenini waliposhinda Mechi 4 na Kufungwa 1 tu na Borussia Dortmund Bao 2-0 kwenye Robo Fainali.

Mechi mbili katika hizo walizoshinda, waliweka Rekodi ya Klabu yao ya Bao nyingi walipozitwanga 6-1 Galatasaray AŞ katika Mechi ya Kundi na FC Schalke 04 katika Raundi ya Mtoano ya Timu 16.

FC Basel 1893 v Liverpool FC

-Msimu wa 2002/03 kwenye Mechi ya Makundi ya UCL, Basel ilitoka Sare 1-1 na Liverpool huko Anfield na katika Mechi ya Marudiano huko Uswisi waliongoza Bao 3-0 lakini Liverpool wakasawazisha na Gemu kwisha 3-3.

KUNDI C

FC Zenit v AS Monaco FC

-Zenit wana Rekodi nzuri Nyumbani kwao Petrovsky Stadium kwa kushinda Mechi 30 kati ya 48 na kupoteza 3 tu katika Kipindi cha Miaka 12.

Bayer 04 Leverkusen v SL Benfica

-Benfica walishinda Mechi zote mbili walipokutana na Bayer 04 Leverkusen Msimu wa 2012/13 wa Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ya EUROPA LIGI kwa kushinda 1-0 huko Germany na 2-1 Nyumbani kwao.

KUNDI D

Arsenal FC v Galatasaray AŞ

-Mara pekee Timu hizi kukutana ni kwenye Fainali ya UEFA CUP Msimu wa 1999/2000 huko Copenhagen, Denmark na kutoka Sare 0-0 katika Dakika 120 za Mchezo na Galatasaray kutwaa Kombe kwa Penati 4-1.

RSC Anderlecht v Borussia Dortmund


-Timu hizi zilikutana kwenye Msimu wa 1990/91 katika Raundi ya Tatu ya UEFA CUP na Anderlecht kufuzu kwa Bao la Ugenini baada kushinda 1-0 Nyumbani na kufungwa 2-1 Ugenini.


RATIBA MECHI ZITAKAZOFUATA

JUMANNE SEPTEMBER  30

KUNDI E

1900 CSKA Moscow VS Bayern Munich
21:45 Man City VS Roma

KUNDI F

21:45 APOEL Nicosia VS Ajax
21:45 Paris St-Germain VS Barcelona

KUNDI G 

21:45 FC Schalke 04 VS NK Maribor
21:45 Sporting Lisbon VS Chelsea

KUNDI H 

BATE Borisovs VS Athletic Bilbao
Shakhtar Donetsk VS FC Porto

Jumatano Oktoba 1

KUNDI A

21:45  Atlético Madrid VS Juvsentus
21:45 Malmö FF VS Olympiakos

KUNDI B 

21:45 FC Basel VS Livserpool
21:45 Ludogorets Razgrad VS Real Madrid

KUNDI C 

1900 Zenit St Petersburg VS Monaco
21:45 Bayer 04 Levserkusen VS Benfica

KUNDI D 

21:45 Arsenal VS Galatasaray
21:45 RSC Anderlecht VS Borussia Dortmund
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment