KIKAO cha Secretarieti ya Coastal
Union kilichoketi jana usiku kimeteua majina ya watu watano watakaosimamia
Uchaguzi Mdogo wa Klabu hiyo unatarajiwa kufanyika Novemba 23 mwaka huu ili
kuweza kuziba nafasi za uongozi zilizokuwa wazi.
Baada ya majina hayo kuteuliwa yatawasilishwa kwenye shirikisho la soka nchini (TFF) kwa ajili ya taratibu nyingine ikiwa ni pamoja na kutangaza tarehe ya uchukuaji fomu na urudishaji.
Baada ya majina hayo kuteuliwa yatawasilishwa kwenye shirikisho la soka nchini (TFF) kwa ajili ya taratibu nyingine ikiwa ni pamoja na kutangaza tarehe ya uchukuaji fomu na urudishaji.
Uchaguzi
huo unafanyika ili kuweza kujaza nafasi tatu zilizokuwa wazi ambazo ni
Mwenyekiti na Wajumbe wawili wa kamati ya utendaji lengo likiwa kuharakisha
maendeleo ya Coastal Union.
Akizungumza mara baada ya kumalizika kikao hicho,Katibu Mkuu wa Coastal Union,Kassim El Siagi alisema kuwa kamati hiyo iliyoteuliwa wana uwezo mzuri wa kusimamia chaguzi mbalimbali mkoani hapa.
“Kimsingi walioteuliwa wana uwezo mzuri lakini lazima majina hayo tuyapelekea TFF kwa ajili ya taratibu nyengine zinazofuata na baadae watae watangaze tarehe ya uchukuaji fomu na urudishwaji fomu tayari kwa ajili ya uchaguzi huo “Alisema El Siagi.
Aliyataja majina yaliyopendekezwa kwenye kikao hicho ambao watakuwa chini ya Mwenyekiti wake Abdallah Yahaya,Katibu Mohamed Awadhi na wajumbe wake watakuwa ni Mtwana Akida Boramini,Ibrahim Khatibu na John Joba.
0 comments:
Post a Comment