JESHI LA POLISI ZANZIBAR LAAHIDI ULINZI WAKATI WOTE WA SIKU KUU YA EDD EL HAJJ ##


Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame
Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame amesema kuwa jeshi la polisi limejipanga kuimarisha ulinzi wakati wote wa sikukuu ya idd el hajj .
Akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba , Kamishna Hamdan amesema kuwa tayari askari wameandaliwa kwa ajili ya kufanya doria sehemu za mijini na vijijini ili kuhakikisha amani inatawala sikukuu hiyo .

Aidha amewataka wazazi kuwalinda watoto wao na matendo hatarishi kwa kutowapa vitu vya thamani na ambavyo vinaweza  kusababisha athari kwa maisha yao watoto .

Kamanda Hamdan ambaye amefuatana na Mkuu wa Operetion wa Jeshi hilo Zanzibar Hassan Nasir amewasisitiza wananchi kuitumia falsafa ya Polisi jamii kwa kuhakikisha kwamba matendo ya uhalifu yanadhibitiwa .

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mh Omar Khamis Othman amewataka wananchi kujiepusha na matendo maovu ambayo yanaweza kusababisha uvunjifu wa amani .

Sala ya idd kifaita ifanyika katika viwanja vya mpira polisi Konde wakati baraza la Idd litafanyika kwenye ukumbi wa Chuo cha Kiislam Micheweni (CSK)  ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Zanzibar DK Ali Mohammed Shein .
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment