Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limekaribisha
wabunifu, kubuni mwonekano wa jezi mpya za timu ya Taifa kwa mechi za nyumbani na
ugenini ambapo mwisho wa kufanya hivyo ni kesho (Novemba 15 mwaka huu). Ubunifu
ni lazima uzingatie rangi za bendera ya Taifa.
Mshindi wa jezi ya nyumbani atapata sh. 1,000,000 (milioni moja),
na mshindi wa jezi ya ugenini atapata pia sh. 1,000,000 (milioni moja).
Ubunifu utumwe kwenye anwani ya barua pepe: info@tff.or.tz
au uwasilishwe kwa CD au flash zikiwa katika mfumo wa PDF katika ofisi za TFF
zilizopo ghorofa ya tatu katika Jengo la PPF Tower, Mtaa wa Ohio na Garden
Avenue.
Kwa maelezo zaidi unaweza kuwasiliana nasi kwa simu namba; 0713
210242 au 0714 634838.
0 comments:
Post a Comment