TIMU
ya Coastal Union imeanza maandalizi kabambe ya kuhakikisha inajipanga vema ili kuhakikisha
timu hiyo inapata pointi tatu muhimu kwenye mechi yake ya Ligi kuu dhidi ya JKT
Ruvu itakayochezwa Jumamosi wiki hii kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani
kutokana na umahiri wa kikosi cha timu hiyo.
Amesema
kuwa mchezo huo utakuwa ni mzuri kwa sababu tayari,Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mkenya
James Nandwa alikwisha fanyia kazi kubwa ya kukiandaa timu hiyo na ataingia kwenye
mechi hiyo akiwa na lengo moja la kuhakikisha ushindi unapatikana ili kuweza kusogea
kwenye nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi kuu soka Tanzania bara.
Hata
hivyo amesema hakuna mchezaji hata mmoja ambaye ni majeruhi na kuwataka wapenzi
na mashabiki kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kwenye mechi hiyo
itakayochezwa kwenye uwanja wao wa nyumbani.
0 comments:
Post a Comment