TAARIFA YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA TANGA KUANZIA MWEZI JANUARI HADI NOVEMBA 2014 ##

Taarifa hii ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga ni utekelezaji mpango kazi wa Jeshi la Polisi kuanzia Januari hadi Novemba 2014, ikionyesha kazi zilizofanywa, matokeo ya kazi hizo na mkakati wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga kukabiliana na uhalifu kwa mwaka 2015.
HALI YA ULINZI NA USALAMA MKOA WA TANGA


Kwa ujumla vitendo vya uhalifu mkoa wa Tanga vimeonekana kupungua kwa baadhi ya makosa na mengine kuongezeka kwa kiwango kidogo kwa kipindi cha Januari hadi Novemba  2014 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013. Huu ni mwendelezo wa kushuka kwa takwimu za uhalifu katika mkoa wetu  tangu mwaka 2006/2007 licha ya kuwepo kwa changamoto kadhaa. Takwimu zilizopo zinaonyesha  kuwa jumla ya matukio yote ya jinai yaliyo ripotiwa Kuanzia Januari hadi Novemba mwaka 2014 ni 17,297, ikilinganishwa na matukio 17,747 yaliyoripotiwa kwa kipindi kama hicho mwaka 2013. Huu ni upungufu wa makosa 450, ikiwa sawa na asilimia 2.53%

Kati ya makosa hayo yaliyoripotiwa Januari hadi Novemba mwaka 2014, Makosa makubwa yalikuwa 2,056 wakati kwa kipindi kama hicho mwaka 2013 yaliripotiwa makosa makubwa 2,124, huu ukiwa ni upungufu wa makosa 68, ikiwa sawa na asilimia 3.20%

Makosa madogo yaliyoripotiwa kuanzia Januari hadi Novemba mwaka 2014 yalikuwa makosa 15,241 wakati kwa kipindi kama hicho mwaka 2013 yaliripotiwa makosa 15,623, huu ukiwa ni upungufu wa Makosa 382, ikiwa sawa na asilimia 2.44%

Kwa mujibu wa takwimu hizo kwa makosa yote yaliyoripotiwa, Makosa dhidi ya Binadamu yaliripotiwa kwa kipindi cha Januari hadi Novemba 2014 ni 7,970 ikilinganishwa na makosa 7,805  katika kipindi kama hicho mwaka 2013 hili ni ongezeko la makosa 165, hii ikiwa ni sawa na asilimia 2.11%.

Makosa ya kuwania mali yaliyoripotiwa kwa kipindi cha Januari hadi Novemba 2014 ni 8,183, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 8,572 , huu ni upungufu wa Makosa 389, hi ni sawa na asilimia 4.53%

Makosa dhidi ya Maadili yaliripotiwa katika kipindi cha Januari hadi Novemba 2014 ni Makosa 1,144 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 1,370, huu ukiwa ni upungufu wa makosa 226, hii ni sawa na asilimia 16.50%

MAKOSA (KESI) MAKUBWA YALIYORIPOTIWA NA JINSI YALIVYOSHUGHULIKIWA
Jumla ya Kesi  kubwa 2056 ziliripotiwa kuanzia Januari hadi Novemba 2014, ambapo Kesi 1031 zipo chini ya upelelezi, Kesi 35 zilifungwa kwasababu mbalimbali za kiupelelezi, Kesi 825 bado zinaendelea Mahakamani, Kesi 156 zilipata ushindi Mahakamani na Kesi 09 Zilishindwa kupata ushindi Mahakamani.
Jumla ya Washtakiwa 1684 walikamatwa kutokana na Makosa hayo makubwa, kati ya hao Wanaume ni 1611 na Wanawake ni 73.

Makosa makubwa ambayo takwimu zinaonyesha yalipungua kuanzia Januari hadi Novemba 2014 ni pamoja na:-
Ø Uvunjaji, ambapo kwa Januari hadi Novemba Mwaka 2014 yaliripotiwa makosa 373, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 381, huu ni upungufu makosa 08 sawa na asilimia 2.09%
Ø Unyang’anyi wa kutumia nguvu, ambapo kwa Januari hadi Novemba Mwaka 2014 yaliripotiwa makosa 91, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 99, huu ni upungufu makosa 08 sawa na asilimia 8.08%
Ø Wizi mkubwa ambapo kwa Januari hadi Novemba Mwaka 2014 yaliripotiwa makosa 03, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 22, huu ni upungufu makosa 19 sawa na asilimia 86.36%
Ø Kubaka ambapo kwa Januari hadi Novemba Mwaka 2014 yaliripotiwa makosa 329, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 337, huu ni upungufu makosa 08 sawa na asilimia 2.37%
Makosa makubwa ambayo takwimu zinaonyesha yameongezeka ni pamoja
Ø Unyang’anyi wa kutumia Silaha ambapo kwa Januari hadi Novemba Mwaka 2014 yaliripotiwa makosa 18, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 10, hii ikiwa ni ongezeko la makosa 08 sawa na asilimia 80%
Ø   Wizi wa Pikipiki ambapo kwa Januari hadi Novemba Mwaka 2014 yaliripotiwa makosa 114, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 71, hii ikiwa ni ongezeko la makosa 43 sawa na asilimia 60%
Ø Wizi wa Mifugo ambapo kwa Januari hadi Novemba Mwaka 2014 yaliripotiwa makosa 364, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 341, hii ikiwa ni ongezeko la makosa 23 sawa na asilimia 6.74%
Ø Mauaji ambapo kwa Januari hadi Novemba Mwaka 2014 yaliripotiwa makosa 100, ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2013 ambapo yaliripotiwa makosa 85, hii ikiwa ni ongezeko la makosa 15 sawa na asilimia 17.64%
Sababu ya kuongezeka kwa makosa haya ni:-
Ø Kuongezeka kwa shughuli za Kiuchumi/ Maendeleo katika maeneo mbalimbali na hasa maeneo ambayo huduma za kiusalama bado ziko mbali hivyo kuongeza vivutio vya uhalifu hasa wa kutumia Silaha.
Ø Mauaji mengi yaliyojitokeza ni kwa sababu ya Wananchi kujichukulia sheria mikononi, na wivu wa Kimapenzi.
Ø Aidha kwa upande wa Pikipiki, kunasababishwa kuongezeka kwa idadi na watumiaji kutochukua hatua za tahadhari za kiulinzi kwa mali zao hizo, jambo linalopelekea kutengeneza mianya inayotumiwa na wezi kuiba Pikipiki.


 HALI YA MWENENDO WA AJALI ZA BARABARANI
Mchanganuo wa takwimu za makosa ya usalama barabarani, mwenendo wa takwimu hizi unaonyesha kuongezeka kwa matukio ya ajali na kupungua kwa matukio ya ajali za vifo.

Mchanganuo wa Matukio ya ajali za Barabarani
Kwa kipindi cha Januari hadi Disemba 26/2014, yaliripotiwa matukio ya ajali za Barabarani 102  ikilinganishwa na matukio  96 yaliyoripotiwa katika kipindi kama hicho 2013 ikiwa ni ongezeko la matukio 06, hii ni sawa na asilimia 6.25%

Ajali za vifo
Kwa kipindi cha Januari hadi Disemba 26/2014, yaliripotiwa matukio ya ajali zilizosababisha vifo 83 ikilinganishwa na matukio  84 yaliyoripotiwa katika kipindi kama hicho 2013 ikiwa ni upungufu wa tukio 01, hii ni sawa na asilimia 1.20%

Idadi ya Vifo
Katika kipindi cha Januari hadi Disemba 26/2014, jumla ya idadi ya watu 116 walikufa kutokana na ajali za barabarani, ikilinganishwa na watu  129 waliokufa kwa kipindi kama hicho mwaka 2013. Huu ni upungufu wa idadi ya watu 13, Sawa na asilimia 10.08%

Idadi ya Majeruhi

Katika kipindi cha Januari hadi Disemba 26/2014, Idadi ya watu waliojeruhiwa kutokana na ajali za Barabarani ni 144 ikilinganishwa na majeruhi 219 kwa kipindi kama hicho mwaka 2013, hii ikiwa ni upungufu wa majeruhi 75, sawa na asilimia 34.25%

Magari yaliyohusika kwenye ajali hizo ni 152 kwa mchanganuo ufuatao:-
Ø Magari Binafsi  -  29
Ø Mabasi               -  24
Ø Malori                -  33
Ø Pick up              -   07
Ø Pikipiki             -   48
Ø Baiskeli             -   11

Jumla ya Makusanyo yote yanayotokana na Notification  kuanzia Januari hadi Disemba 26/2014 ni Tshs.1,054,740,000/= ukilinganisha na muda kama huo mwaka 2013 ambapo makusanyo yote yalikuwa Tshs. 801,846,000/= hili likiwa ni ongezeko la Tshs 252,894,000/= sawa na asilimia 32%

Magari yaliyokaguliwa kwa Kipindi cha Januari hadi 26/2014 ni  Magari 16,143

USHIRIKI WA POLISI JAMII KATIKA ULINZI NA USALAMA

Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga kupitia kitengo cha Polisi jamii kwa kushirikiana na Wakaguzi tarafa na Polisi Kata  tumefanikiwa kutengeneza mahusiano / ushirikiano mzuri na wadau mbalimbali kutoka kwenye jamii inayotuzunguuka kama vile wafanyabiashara wakubwa na wadogo, viongozi wa ngazi mbalimbali za serikali, wabunge, madiwani, viongozi wa madhehebu ya dini na wananchi kwa  ujumla.

Uhusiano huu unatusaidia kuratibu ushiriki wa wananchi katika swala zima la ulinzi na usalama katika himaya zao kwa kuhimiza kuanzishwa kwa kamati za ulinzi na usalama kwenye makundi ya kijamii, kwa mfano kwenye Nyumba za ibada, maeneo ya biashara, maeneo ya makazi ya watu na Vikundi vya ulinzi shirikishi.

Mchanganuo wa Kamati za ulinzi na vikundi vya ulinzi kwenye makundi mbalimbali ya jamii ni kama inavyoonekana kwenye Jedwali;
JEDWALI LIKIONYESHA IDADI YA KAMATI ZA ULINZI NA USALAMA NA VIKUNDI VYA ULINZI SHIRIKISHI KWENYE  MAENEO YA MAKUNDI YA KIJAMII -KIWILAYA.
WILAYA
KAMATI ZA ULINZI KWENYE NYUMBA ZA IBADA
KAMATI ZA ULINZI KWENYE MAENEO YA BIASHARA
VIKUNDI ULINZI KWEYE NYUMBA ZA IBADA
VIKUNDI  VYA ULINZI KWENYE MAENEO YA BIASHARA
VIKUNDI VYAULINZI KWENYE MAKAZI
TANGA
05
01
05
01
08
MKINGA
02
06
02
06
10
PANGANI
03
12
02
02
12
KILINDI
03
02
-
-
07
KOROGWE
14
08
07
11
97
MUHEZA
50
06
12
07
46
HANDENI
04
04
-
03
06
LUSHOTO
08
28
08
21
157
JUMLA
89
67
36
51
338


Aidha elimu ya ukamataji salama, namna ya kufanya doria, utoaji wa taarifa, namna ya kushuku na haki za wale wanao washuku na kuweza kuwa kamata na mipaka yao kiutendaji imeendelea kutolewa kwa Askari wa Vikundi vya ulinzi shirikishi kwa Wilaya zote nane za Mkoa wa Tanga, ambapo Jumla ya Askari wa Vikundi vya ulizi shirikishi 400 walipatiwa mafunzo hayo na kati ya hao Askari 250 walipatiwa vyeti huko Wilaya ya Kilindi na wengine waliobakia mpango unaendelea wa kuwapatia vyeti.

Elimu ya ulinzi kwenye malindo imetolewa kwa Askari wa Makampuni ya Ulinzi yaliyoko Jiji la Tanga ambapo Jumla ya Askari 40 walipatiwa mafunzo ya Ukakamavu na ulinzi wa kwenye malindo.  

Katika kutekeleza mwongozo wa kusogeza huduma za Kipolisi karibu na Wananchi, Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga tayari tumeunda Vikosi kazi vya Kipolisi katika Tarafa zote 37 zilizoko Mkoa wetu wa Tanga.

Kupitia Mfuko wa Wafanyabiashara dhidi ya uhalifu Mkoa wa Tanga (Tanga Region Business Fund Against Crime) kwenye Kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa New kwetu Hotel kulipangwa mkakati wa kuiboresha Karakana ya Polisi iliyoko Kambi ya Polisi Mabawa, kununua Pikipiki za doria za Polisi, kuendelea kuwapatia posho ya kujikimu kwa Mgambo 20 wanaofanya kazi katika Vituo vidogo vya Polisi.  


MATISHIO YA USALAMA MKOA WA TANGA
Mkoa wetu wa Tanga unazo changamoto za Matishio ya Kiusalama ambazo zinatokana na mazingira ya  Kijiografia, Kijamii, Kiuchumi, na Kiutamaduni, changamoto hizo ni pamoja na;
Ø Matishio ya Uhalifu wa Kimataifa kama vile Usafirishaji haramu wa Binadamu, Usafirishaji na matumizi ya Madawa ya kulevya ya Viwandani na Mashambani pamoja na matishio ya Ugaidi.
Ø Migogoro ya ya Kijamii kama vile,
·        Migogoro ya Ardhi kati ya Wakulima na Wafugaji hasa kwenye Wilaya za Kilindi, Korogwe, Handeni, Pangani na kwa kiwango kidogo maeneo ya Mkinga.
·         Migogoro ya ardhi kati ya Wawekezaji wa Mashambani na Wenyeji wanaozunguka maeneo hayo, kwenye Wilaya za Muheza, Lushoto, Korogwe
·        Mgogoro wa Ardhi kati ya Wachimbaji wadogo wa Madini na Makampuni yaliyomilikishwa maeneo hayo kisheria. Wilaya za Handeni, Korogwe na Muheza.
Ø  Uharibifu wa Mazingira kwa ukataji miti hovyo hasa eneo la Mwakijembe Wilaya Mkinga na uvuvi Haramu.
Ø Changamoto za upana wa Mpaka kuweza kudhibiti na kuzuia uhalifu unaovuka mpaka kwani zipo Bandari Bubu zaidi ya hamsini  na njia nyingi zisizo rasmi (Panya road) hivyo kupelekea changamoto kubwa sana kiusalama.

MIKAKATI YA KUKABILIANA NA UHALIFU KWA MWAKA 2015
Katika kupambana na Uhalifu, Migogoro mbalimbali na Majanga, tumejiwekea utaratibu kama ifuatavyo;
ü Kuishirikisha Jamii katika kuzuia na kupambana na uhalifu kwa kutumia Viongozi wa Serikali za Mitaa na Vijiji kusimamia mpango wa ulinzi shirikishi kwa kutoa taarifa na kuhuisha Vikundi vya ulinzi shirikishi.
ü Kuhamasisha matumizi ya Daftari la Makazi ili kubaini Wageni wanaoingia na kuweza kuwafuatilia nyendo zao ikiwa ni pamoja na sababu za uwepo wao.
ü Kuimarisha usalama kwenye maeneo ambayo yameonekana kuwa na tatizo kubwa la kiuhalifu kwa kuimarisha doria na misako ya ghafla.
ü kuwapima madereva wanaoendesha magari yanayosafiri kwenda nje ya Mkoa wa Tanga kama wana kilevi kila wanapoondoka Stand Kuu.
ü Kutoa elimu ya matumizi sahihi ya Barabara kwa wakazi wanaokaa kwenye Vijiji vilivyoko kando kando ya Barabara Kuu za Mkoa.
ü Kuwasiliana na Maafisa Mifugo ili kutumia utaratibu wa kutoa vibali kwa mtu anayetaka kuuza au kusafirisha mifugo yake, hii ikienda sambamba na kuwasiliana na Serikali za Vijiji kulisimamia vyema zoezi la vibali hivyo,  ili kuwakamata wezi wa mifugo kiurahisi.
ü Kutumia Wakaguzi Tarafa na mfumo wa Polisi Kata kwa ujumla kama vyanzo muhimu vya taarifa zinazoonyesha dalili za awali za kuwepo kwa Uhalifu au mgogoro wa makundi fulani ya jamii na kuyashughulikia mapema kwa kushirikaiana na wadau wengine. 

ü Kuendelea kutoa Elimu ya kutosha kwa askari wetu, hususani katika chumba cha mashitaka kubaini taarifa zinazopokelewa kituoni ili zile zenye mwelekeo wa migogoro baina ya makundi fulani ya jamii, zifikishwe kwa viongozi mara moja ili zishughulikiwe haraka.

ü Polisi Mkoa wa Tanga tutahakikisha kwamba Wananchi wanendelea kupata huduma bora na kwa wakati licha ya kuwepo changamoto mbalimbali. Pia kwa Askari watakao fanya kazi zao vizuri watazawadiwa na wale ambao watafanya kazi vibaya na kukiuka maadili ya Polisi wataadhibiwa ipasavyo kwa mujibu wa Kanuni na Sheria zilizopo. Kwa mwaka 2014 Askari 16 walioadhibiwa kutokana na utovu wa nidhamu na kupewa adhabu mbalimbali.


ü Kutoa Elimu kwa pande zilizo katika migogoro juu ya hatua za kisheria zifaazo kuchukuliwa ili kufikia ufumbuzi wa kudumu wa migogoro husika na kupitia Askari Kata, kuendelea kufuatilia hatua za utatuzi wa migogoro hiyo katika vyombo husika, ili kuendelea kushauri nini zaidi chakufanya kama rufaa badala ya kuchukua sheria mkononi.
HITIMISHO
Tunatoa shukrani za dhati kwa Makundi mbalimbali ya Jamii ya Wakazi wa Mkoa wa Tanga  kwa ushirikiano wao mkubwa walioutoa kwa Jeshi la Polisi na kuendelea kuufanya mkoa wetu kuwa shwari, ni wito kwa Jamii kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuzuia na kupambana na uhalifu ili kuleta maendeleo katika mkoa wetu kwani bila usalama hakuna maendeleo.
Tunatoa tahadhali kwa wale wote ambao wanajihusisha vitendo vya uhalifu waache mara moja kwani tumejipanga vizuri kwa kushirikiana na Jamii kukabiliana nao, hatutakuwa na mzaha wala huruma kwa Mhalifu yoyote, wajuwe kwamba siku zao zinahesabika.
Aidha  Tunatoa shukrani za Dhati kwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tanga chini ya Uongozi wa aliyekuwa  Mkuu wa Mkoa wa Tanga Lt. Chiku Galawa na Mkuu wa Mkoa wa sasa Mheshimiwa Magalula Said Magalula kwa miongozo na ushirikiano mkubwa walioutoa kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga kwa kipindi chote cha kuanzia Januari hadi Disemba 26/2014.
NAWATAKIA HERI YA MWAKA MPYA 2015 WENYE AMANI NA UTULIVU

IMETOLEWA NA  (FRASSER KASHAI-SACP)
KAMANDA WA POLISI MKOA WA TANGA
Share on Google Plus

About trustedmishen

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment